Hebu tuzungumzie juu ya sheria. Paulo Mtumie aliwaambia Wayahudi walio ifuata sheria “kwa hiyo wewe mtu uwaye yote uhukumuye, huna udhuru, kwa maana katika hayo umhukumuye unafanya yale yale: Nasi twajua ya kuwa hukumu ya Mungu ni ya kweli juu yao wafanyao hayo. Wewe binadamu uhukumuye je, wadhani ya kwamba utajiepusha na hukumu ya Mungu?” (Warumi 2:1-3). Waifuatao sheria hudhani kwamba wao ndio wanao mheshimu Mungu zaidi. Aina hii ya watu hawamwamini Mungu kwa mioyo yao yote, bali kwa majivuno yao bandia yaliyo katika msingi wa matendo yao. Watu hawa hupenda kuwahukumu wengine na ni wepesi kwa hilo sana. Hata hivyo wakiwa wana wahukumu wengine kwa maneno ya Mungu hawagundui ya kwamba wao nao wanafanana na hao wanao wahukumu na pia kufanya makosa hayo hayo.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Je, unaifahamu na kuiamini siri ya ubatizo wa Yesu alio upokea toka kwa Yohana? Ningependa kukueleza juu ya siri hiyo kupitia Warumi 6:1-4 “Tuseme...
Nampa Bwana shukrani kwa kuokoa nafsi nyingi nyakati hizi. Biblia inazungumiza juu watu walio na heri katika Warumi sura ya 4, hivyo ningependa kuzungumiza...
Imeandikwa “Mwenye haki ataishi kwa imani” Je, tunaishi kwa imani au la? Njia pekee ya mwenye haki kuishi ni kwa imani. Imani ndiyo imwezeshayo...